Akijielezea kama mkate wa uzima, Bwana wetu alisema, “Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu,kwa ajili ya uzima wa ulimwengu” (Yohana 6:51). Kisha aliendelea kusema, “Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake,hamna uzima ndani yenu.Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele;nami nitamfufua siku ya mwisho.Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu,nami ndani yake.” (Yohana 6:53-56). Waliposikia hayo, hata Yesu mwenyewe alisema, Hili ni neno gumu; nani anaweza kuielewa? Tunakula mwili wa Yesu na kunywa damu yake kwa kuamini injili ya maji na Roho. Ni wakati tunapo kula mwili wa Bwana ndipo mioyo yetu huondolewa dhambi. Kwa maneno mengine, mtu ye yote anayekula mwili wa Bwana amekuwa hana dhambi kabisa, na dhambi zote nyingi katika moyo wake zilifutwa.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Yesu alitupa uzima wa milele kwa sisi ambao ni wenye haki. Inamaanisha kwamba ametupa uzima wa kuishi milele chini ya upendo na baraka zake...
Yohana sura ya sita ni ngumu kueleweka kwa Wakristo leo pia. Kwa hivyo hata wachungaji hawapati mahubiri yoyote kwenye kifungu hiki. Kawaida wanatafsiri ujumbe...
Wakati Yesu alipanda mlimani na kuhubiri, umati wa watu ulikuwa ukimfuata. Kisha akiweka mikono Yake juu ya chakula kidogo ambacho kilikuwa cha kutosha kwa...